Psalms 86

Kuomba Msaada

(Maombi Ya Daudi)


1 aEe Bwana, sikia na unijibu,
kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.

2 bLinda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako,
wewe ni Mungu wangu,
mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.

3 cEe Bwana, nihurumie mimi,
kwa maana ninakuita mchana kutwa.

4 dMpe mtumishi wako furaha,
kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana,
ninainua nafsi yangu.


5 eEe Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe,
umejaa upendo kwa wote wakuitao.

6 fEe Bwana, sikia maombi yangu,
sikiliza kilio changu unihurumie.

7 gKatika siku ya shida yangu nitakuita,
kwa maana wewe utanijibu.


8 hEe Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe,
hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

9 iEe Bwana, mataifa yote uliyoyafanya
yatakuja na kuabudu mbele zako;
wataliletea utukufu jina lako.

10 jKwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu;
wewe peke yako ndiwe Mungu.


11 kEe Bwana, nifundishe njia yako,
nami nitakwenda katika kweli yako;
nipe moyo usiositasita,
ili niweze kulicha jina lako.

12 lEe Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote;
nitaliadhimisha jina lako milele.

13 mKwa maana upendo wako ni mkuu kwangu;
umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi.
Yaani Kuzimu.


14 oEe Mungu, wenye majivuno wananishambulia;
kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu:
watu wasiokuheshimu wewe.

15 pLakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema,
si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.

16 qNigeukie na unihurumie;
mpe mtumishi wako nguvu zako,
mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
Au: mwokoe mwanao mwaminifu.


17 sNipe ishara ya wema wako,
ili adui zangu waione nao waaibishwe,
kwa kuwa wewe, Ee Bwana,
umenisaidia na kunifariji.
Copyright information for SwhKC